Ile Mixtape Kutoka Marekani ya Coast2coast yenye wimbo wa Gosby ‘BMS’ yatoka, idownload hapa

Wimbo Gosby, BMS imeweka historia kwa kuwa wimbo pekee kutoka Africa Mashariki na Kati kuweza kuingia kwenye (mixtape) no1 duniani ya Coast 2 Coast ya nchini Marekani.


BMS ni wimbo number 12 kwenye play list yenye takribani nyimbo 22 tu zilizopata nafasi ya kuingia kwenye mixtape hiyo baada ya kupigiwa kura na mashabiki wa muziki wa hiphop duniani . Fursa hii itampa Gosby nafasi ya wimbo wake wa BMS kusambazwa kwa wadau na wapenzi wa muziki zaidi ya 2,000,000 duniani. Coast2Coast Mixtape Vol 251 imetoka tarehe 21/12/2013





PENGINE UTAKUWA UNAJIULIZA COAST 2 COAST NI NINI?


Coast2Coast ni kampuni ya kimarekani inayojishughulisha na utayarishaji, usambazaji na promosheni za mixtapes duniani. Coast 2 Coast mixtapes ni mixtape zinazokuwa downloaded kwa wingi zaidi Duniani. Coast 2 Coast mixtapes zimepata zaidi ya downloads Million 200 tangu zilipoanzishwa miaka kadhaa iliyopita.


Miongoni mwa wasanii ambao wameshawahi kufanya kazi na Coast 2 Coast mixtapes ni pamoja na 50 cent, Snoop Dogg, Wiz Khalifa, Big Sean, Game, Pharell, Nas, Lupe Fiasco, Chris Brown, LL Cool J, Fabolous, Gym Class Heroes, Flo Rida na wengine wengi, Vile vile ma dj kama Dj Drama, Dj Khaled, Bigga Rankin, Dj Ill Will na wengine wengi.
Kila toleo la mixtape za Coast 2 Coast husambazwa kwa watu zaidi ya milioni 1.2 duniani na hupostiwa kwenye zaidi ya websites/blogs 1000 maarufu za muziki duniani ambazo kwa ujumla hupata downloads zaidi ya 500,000 kila toleo. Vilevile kila toleo husambazwa na wasambazji zaidi ya 400 ambao husambaza copies katika majimbo kadhaa nchini Marekani, Africa na Ulaya.

JINSI YA KUDOWNLOAD

Ingia kwenye link hii:- c2c.fm/f8QBb



Previous Post Next Post