WANAMUZIKI WALIOINGIZA PESA NYINGI ZAIDI 2013, MODONNA AKAMATA NAFASI YA KWANZA ICHEKI LIST NZIMA HAPA

Jarida la Forbes limetoa orodha mpya ya wanamuziki walioingiza pesa nyingi zaidi kwa miezi 12 iliyopita, na Madonna ndiye amekamata nafasi ya kwanza.




Kwa mujibu wa jarida hilo, Madonna mwenye miaka 55 ametengeneza kiasi cha dola milioni 125 kuanzia June 2012 hadi May 2013, chanzo kikubwa kikiwa ni tour yake ya MDMA.

Jarida hilo limesema kuwa limezingatia zaidi mauzo ya tiketi katika tour, mirahaba ya nyimbo, dili za endorsements, pamoja na biashara zake zingine kama clothing line, na perfume vyote vikiweka mchango katika kumfanya awe mwanamuziki aliyeingiza pesa zaidi 2013 kwa mujibu wa Forbes.


Mwanamuziki mwenye vituko hasa katika uvaaji wake Lady Gaga amekamata nafasi ya pili katika orodha hiyo akimfuatia Madonna. Gaga ameingiza dola za Marekani milioni 80 kwa mwaka.

Nafasi ya tatu imekamatwa na Bon Jovi aliyeingiza $79 million kwa mwaka mzima ambayo pia imetokana na tour aliyoifanya, na mauzo katika concert zake.


Justin Bieber amekamata nafasi ya sita kwa kuingiza dola milioni 58 kutokana na uwekezaji alioufanya Enflick, Tinychat na Spotify.

Taylor Swift amekamata nafasi ya saba kwa kuingiza $55 million kwa mwaka alizozipata kwa msaada wa dili za endorsement alizosaini.

Sir Elton John amekamata nafasi ya nane kwa kuingiza $54 million akifuatiwa na Beyonce pamoja na Kenny Chesney waliokamata nafasi ya tisa na kumi wakiwa wameingiza $53 million kila mmoja.



Staa wa Bad Boy Records Diddy amekamata nafasi ya 11 kwa kutengeneza 50 million, Jennifer Lopez nafasi ya 14 kwa kuingiza $45 million na Rihanna nafasi ya 17 kwa kuingiza $43 million huku Jay Z akikamata nafasi ya 18 kwa kuingiza $42 million.

Tazama orodha nzima

1. Madonna $124 million
2. Lady Gaga $80 million
3. Bon Jovi $79 million
4. Toby Keith $65 million
5. Coldplay $64 million
6. Justin Beiber $58 million
7. Taylor Swift $55 million
8. Elton John $54 million
9. Beyonce’ $53 million
10. Kenny Chesney $53 million
11. Diddy $50 milliom
12. Paul McCartney $47 million
13. Calvin Harris $46 million
14. Jennifer Lopez $45 million
15. Roger Waters $44 million
16. Muse $43 million
17. One Direction $42 million
18. Jay Z $42 million
19. Rolling Stones
20. Red Hot Chili Peppers $40 million
21. Katy Perry $38 million
22. Tim McGraw $33 million
23. Pink $32 million
24. Tiesto $32 million
Previous Post Next Post