Q-CHILLA AFUNGUKA JUU YA KESI YA BABU SEYA: WASANII WA BONGO WALIPASWA KUTOA KAULI ZAO KWENYE RUFAA YA BABU SEYA

Q-Chilla amesema amesikitishwa na jinsi wasanii wenzake walivyokuwa kimya kwenye rufaa ya Babu Seya na Papii Kocha ambao rufaa yao imekataliwa leo na hivyo kuendelea na kifungo cha maisha jela.




Hit Maker uyo wa Wimbo wa ‘Beautiful'  Q-Chilla amesema kama kungekuwepo na kauli za wasanii kuhusiana na rufaa hiyo huenda mambo yangekuwa tofauti.

“Wameshindwa, wamekaa tu kufanya kazi zao za kujipromote wao, this is very stupid,” amesema Chilla.

“Kauli yao tu ni faraja kwa hawa jamaa. Wangeona kuna watu kule nje hata kama hawana uwezo wa kututoa au kuiambia serikali itutoe, kwamba kuna watu kweli wako touched na hii issue. Always wanasubiri mtu afe au jambo hili litokee, ndio wajitokeza wazungumze. Nahisi kila mtu anaishi sababu anafanya kazi zake na afulfill dreams zake, but we are not there for other people who need hata kauli zetu. Ukizungumza unaonekana una stress. Ila Mungu ana sheria zake na serikali ina sheria zake. Nimekubaliana na hilo.”
Previous Post Next Post