HUYU NDIYE MSANII WA BONGO FLAVOUR AMBAYE BABA YAKE ANA UMRI MKUBWA KULIKO WASANII WOOTE WA BONGOFLAVOUR



Ukimuona Timbulo akiwa na baba yake, ni rahisi kuwa na imani kuwa huyo ni babu yake kutokana na Uzee wake. Ukweli ni kwamba, baba mzazi wa msanii huyo, ana umri wa miaka 107. Akiongea kwenye kipindi cha Sunrise cha Times FM, leo, Timbulo alisema wazazi wake wamekuwa wakiugua mara kwa mara kutokana na umri wao. Katika hatua nyingine, leo ni siku ya kuzaliwa ya mama yake mzazi, ambaye hata hivyo mama yake huyo hakumbuki mwaka aliozaliwa. Kupitia Instagram, Timbulo ameandika: “Kiukweli upendo wako kwangu ni unreplaceable, cjapata na am sure cwez kupata mwanamke mwenye upendo wa dhati kama ule unaonipa, furaha na nuru hii hugeuka huzuni na giza kila nikifikiri cku utakayoniacha ntakuwa katika hali gani, daaaaah mola nipe la hili swali maana,,,, happy birthday mama yangu mie japo umri na muonekano wako ni kama bibi yangu na hata umri wako hujui ni miaka mingapi ila cwez kuubadili ukweli huu ur my mother, am proud of n I love u so much.”
 
Source: Times Fm 

Previous Post Next Post