Kutoka kwa Obama: Eminem na Lady Gaga kutumbuiza kwenye Youtube Music Awards



Eminem na Lady Gaga wamepangwa kutumbuiza kwenye uzinduzi wa YouTube Music Awards mwezi ujao.






Kwa mujibu wa The Hollywood Reporter, show hiyo ya dakika 90 itafanyika New York City, Nov. 3 na itaoneshwa live mtandaoni. Mtengenezaji wa filamu, Spike Jonze, aliyeongoza video za muziki za Kanye West na Jay Z, atakuwa Mkurugenzi wa Ubunifu wakati Jason Schwartzman akohost. YouTube Music Awards zitawapa heshima wasanii na nyimbo ambazo watumiaji wa YouTube wamezifanya ziwe hits miaka iliyopita. Majina ya watakaowania tuzo hizo yatatangazwa Oct. 17, kuzingatia umaarufu wa video.
Previous Post Next Post