Picha: Huyu Ndiye Mshindi wa taji la Miss World 2013 ni Megan Young Kutoka Plilinino



Miss Ufilipino, Megan Young, jana aliibuka mshindi wa Miss World 2013 kwenye fainali zilizofanyika katika kisiwa cha Bali nchini Indonesia ambako kulikuwa na ulinzi mkali.
fe2a8268b8dbae203e0f6a70670051e5

Megan Young, Miss World 2013
“Naahidi kuwa Miss World bora zaidi,” Young mwenye miaka 23, alisema baada ya kushinda fainali hizo za 63 wakati ambapo Wafilipino kibao waliokuwa wamesafari kwenda kushuhudia fainali hizo wakisherehekea kwa kurukaruka na kupeperusha bendera ya nchi yao kwa furaha.
0ed9e275b8ddaf203e0f6a706700bf2d
Licha ya kuwepo vitisho kutoka kwa kundi la Islamic Defenders Front kuwa lingeshambulia shindano hilo, polisi walisema hakuna maandamano yaliyofanyika jana. Warembo 127 walishiriki kwenye shindano hilo.
0e6e152b-1aab-4b38-a66b-6528453a12da_AP436786033592

Kutoka Kushoto: Miss Ufaransa, Marine Lorphelin, 20, aliyekamata nafasi ya pili, Megan Young na Miss Ghana, Carranzar Naa Okailey Shooter, 22, aliyekamata nafasi ya tatu
557a383337ef0cbeeaaa16d3478a435d8c79f26a

Mshindi wa mwaka jana, Wenxia Yu wa China, akiwa amemkumbatia mrithi wake
2013-09-28T211538Z_202280279_GM1E99T0E6N01_RTRMADP_3_INDONESIA-MISSWORLD

Megan ameshaigiza filamu zaidi ya 10 nchini Ufilipino zikiwemo The Reunion na Bang Bang Alley
Young, aliyemrithi mshindi wa mwaka jana, Wenxia Yu wa China, alizaliwa nchini Marekani. Alipokuwa na miaka 10 alirudi kwao Ufilipino ambako ameonekana kwenye filamu na kufanya kazi kwenye TV.
cc1f37e437fa341e0eaac51b53e9517a7d107300
0f94f732b7b2a9203e0f6a7067002c2b

Zaidi ya polisi 700 walimwagwa kuhakikisha usalama wakati wa fainali hizo
ab181b15b7b2a9203e0f6a70670004f5


Previous Post Next Post