Mkataba Mnono: JB, Steve Nyerere na Bi. Kiroboto waingia mkataba wa matangazo na Airtel



Wasanii wa filamu nchini Jacob Stephen aka JB,Steve Nyerere na Bibi Kiroboto wameingia mkataba mnono wa matangazo na kampuni ya Airtel utakaudumu kwa muda wa mwaka mmoja.

page
Akiongea na Bongo5, Steve Nyerere amesema wameanza na mkataba wa mwaka mmoja ambapo watafanya matangazo ya kampuni hiyo kuanzia kwenye mabango ya barabarani, redioni na kwenye runinga.
Hata hivyo Steve hajaweka wazi kiwango alicholipwa kutokana na mkataba huo wa kufanya matangazo ya Airtel Yatosha. Tayari barabarani kuonekana mabango yenye sura za wasanii hao.
Previous Post Next Post