MAMA ASHA BILAL AADHIMISHA SHEREHE ZA MIAKA 10 YA TAASISI YA MAZNAT NA KUZINDUA SHULE YA UREMBO YA TAASISI HIYO




 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana jioni kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, kama Mgeni rasmi sambamba ya kuzindua Shule ya Taasisi hiyo inayofundisha masuala ya urembo.
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akishiriki kukata Keki na Maza Sinare, ambaye ni mmiliki wa Saluni ya Maznat, ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana Mei 5, 2013, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo. 
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
 Mama Asha, akipongezwa na wageni waalikwa baada ya kusoma hotuba yake ukumbini hapo.
 Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe hizo.
 Mmiliki wa Saluni na Taasisi ya Maznat, Maza Sinare, akiwalisha keki baadhi ya wageni waalikwa wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam jana, sambamba na sherehe hizo pia Mgeni rasmi mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal (kulia) akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi shule ya masuala ya Urembo, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana. Shule hiyo inasimamiwa na Taasisi hiyo.luni na Taasisi hiyo ya Maznat, Maza Sinare.
 Msanii wa muziki wa Taarab, Mzee Yusuph, akiimba jukwaani kutoa burudani wakati wa sherehe hizo.
 Mama Asha Bilal, akiwaongoza wanawake waliohudhuria sherehe hizo katika kucheza muziki wa taarab, burudani iliyokuwa ikitolewa ukumbini hapo na Mzee Yusuph.
 Msanii wa muziki wa Injili, Bahati Bukuku, akiimba jukwaani kutoa burudani wakati wa maadhimisho hayo.
 Baadhi ya wadau wa Maznat, waliohudhuria sherehe hizo, wakisebeneka na miondoko ya taarab, ukumbini hapo.
 Baadhi ya wadau wa Maznat, waliohudhuria sherehe hizo, wakisebeneka na miondoko ya taarab, ukumbini hapo.
 Baadhi ya wadau wa Taasisi ya Maznat, wakihesabu fedha zilizopatikana baada ya kuchangwa na washirika wa karibu wa Taasisi hiyo ukumbini hapo jana wakati wa sherehe hizo kwa ajili ya kusaidia mfuko wa kusaidia Watoto Yatima ulio chini ya Taasisi hiyo, ambapo zilipatikana jumla ya sh. milioni 15, 500, 7200 
 Mmiliki wa mtandao wa Mafoto Jr, Nasma Mafoto (kushoto) akiwa na wadau waliohudhuria sherehe hizo.
 Wasanii wa kundi la The Voice, wakitoa burudani ya kuimba 'Akapera' jukwaani wakati wa sherehe hizo.
 Mabaunsa wakifungua na kuripua Shampeni kwa pamoja ikiwa ni sehemu ya kusherehesha ukumbini hapo.
 Maznat, akipozi kwa picha na wafanyakazi wake...
 Mama Asha Bilal, akiwaongoza wageni waalikwa kugonganisha glasi wakati wa sherehe hizo.
 Kwa amani na furaha ya kutimiza miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, wageni waalikwa waligonganisha glasi zao.
Previous Post Next Post

Popular Items