![]() |
Pope Francis I |

*Ni mtu wa kwanza katika kipindi cha miaka elfu moja kwa mtu kutoka nje ya bara la Ulaya kutawazwa kuwa papa wa Kanisa Katoliki.
*Ni mzaliwa wa Buenos Aires huko Argentina mwaka 1936.
*Ni muitaliano aliyekuwa akifanya kazi katika shirika la Usafiri wa Treni kabla ya kuhamia nchini Argentina miaka ya zamani.
*Kadinali Bergoglio amekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya Argentina.
*Ana umri wa mwaka 76, na kwa miaka yake yote kama Kasisi amehudumu nyumbani kwao Argentina.
*Inasemekana kuwa yeye ndiye aliyeibuka nambari mbili katika uchaguzi wa Papa mwaka 2005 Papa Benedict XVI aliposhinda.
![]() |
Moshi mweupe ulioashiria Papa amepatikana |
*Anaaminika kuwa na ujuzi mkubwa ambao wengi wanasema utamsaidia sana katika uongozi wake.
*Bergoglio ameibuka kuwa mtu anayependa sana udhabiti wa kisiasa katika nchi zilizo katika bara la Amerika Kusini.
*Bergoglio anasifiwa kwa kuleta mageuzi makubwa katika Kanisa la Argentina pamoja na kushikilia misingi.
![]() |
Pope Francis I akiongea na waumini mara baada ya kuchaguliwa |