Lady Jaydee awa balozi wa uzazi wa mpango

Mwanamuziki Lady Jaydee ametuliwa na Hospitali ya Marie Stopes kuwa balozi wa kampeni ya kuhamasisha uzazi wa mpango na kupinga mimba za utotoni inayoitwa ‘Chagua Maisha’.

Akiongea na TBC, Lady Jay Dee amesema kuwa anaweza kufikisha ujumbe kwa jamii kwa kuimba nyimbo ambazo zitasaidia kuwahamasisha wananchi kuchagua jinsi ya kuishi kwa kutumia uzazi wa mpango.


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marie Stopes Tanzania (MST), Uller Muller (kulia) akikabidhi kisanduku chenye vifaa vinavyohusika na masuala ya uzazi wa mpango kwa Balozi mpya wa Marie Stopes ambaye pia ni msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura ‘Lady jaydee’ katika hafla ya utiaji sahihi makubaliano hayo katika ofisi za MST, jijiji Dar es Salaam jana.

Previous Post Next Post