Lady Jay Dee na Diamond platnumz washinda tuzo za AFRIMMA 2014, Orodha Kamili iko hapa

Wasanii wa Tanzania wenye mashabiki wengi Afrika Mashariki, Lady Jay Dee na Diamond Platinumz, wameitoa Tanzania Kimasomaso kwa kushinda tuzo moja moja katika tuzo za AFRIMA (African Muzik Magazine Awards 2014), zilizofanyika jana Dallas, Marekani.

Kwa mujibu wa mtandao wa African Music Magazine, Lady Jay Dee alishinda tuzo ya mwimbaji bora wa kike wa Afrika Mashariki na Diamond Platinumz alishinda tuzo ya Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki.

Hata hivyo, kwa habari ambazo zimeenea Tanzania na kutajwa kuwa zilizotolewa na meneja wa Diamond zinaeleza kuwa Diamond ameshinda tuzo mbili ambayo nyingine ni wimbo bora wa kushirikiaha.

Lakini kwenye orodha halisi ya mtandao a AFRIMMA, tuzo ya wimbo bora wa kushirikiana imeenda kwa Mafikizolo feat Uhuru (Khona).



Kwa mujibu wa maelezo aliyoandika Diamond kwenye Instagram, inaonesha kama ameshinda tuzo zaidi ya moja.

“First of all napenda nimshkuru sana Mwenyez mungu, Mama, Family, My management, kipenzi changu, Media, bila kuwasahau nyinyi mashabiki zangu pendwa kwani sikuzote mmekuwa mkinisupport bega kwa bega kwenye shida na raha...Niwashkuru pia Wasanii wenzangu toka nje na ndani ya Tanzania kwani naamini changamoto tunazopeana ndio zimefanya hadi sasa mziki wetu ufikie hapa...hakika tunzo hizi si zangu bali ni za Muziki wa Bongo flavour... Mwisho kabisa nimshkuru Mh Rais Jakaya Mrisho kikwete kwa mchango wake wa kila siku katika sanaa yetu!... Mr President your Son Did it!!!!! #MdogMdogo.”



Hii ni orodha kamili ya washindi wa AFRIMMA 2014

Best DJ Africa 2014- Dj Black (Ghana)

Best African DJ USA 2014 – Dj Josh (Kenya)

Best Video of the Year 2014- Flavour (Nigeria)

Best Male East Africa 2014- Diamond (Tanzania)

Best Male West Africa 2014- Davido (Nigeria)

Best Female East Africa 2014- Lady Jaydee (Tanzania)

Best Female West Africa 2014 – Tiwa Savage (Nigeria)

Best Male Central Africa 2014 – Fally Pupa (Congo)

Best Female Central Africa 2014- Gasha ( Cameroon)

Best Male Southern Africa 2014- Khuli Chana (South Africa)

Best African Group 2014- P-square (Nigeria)

Best Male Diaspora 2014- Fuse ODG (Ghana)

Best Female Diaspora 2014- Les Nubians (Cameroon)

Best Female Southern Africa 2014- Zahara (South Africa)

Best Dancehall Artist 2014 – Timaya (Nigeria)

Best Dance in a Video 2014- Iyanya (Lekwa Ukwu) (Nigeria)

Best Gospel Artiste 2014- Bahati (Kenya)

Best Traditional Artist 2014- Flavour (Nigeria)

Best Newcomer 2014- Stanley Enow (Cameroon)

Best Video Director 2014- Ogopa Dj’s (Kenya)

Music Producer of the year 2014- Dj Oskido (South Africa)

Best Dance Group 2014- Imagineto (Nigeria)

Best Rap Act 2014- Sarkodie (Ghana)

Best Collaboration 2014- Mafikizolo ft Uhuru (Khona) (South Africa)

Song of the Year 2014- Kcee (Nigeria)

Artist of the Year 2014- Davido (Nigeria)

Leadership in Music Award 2014- 2face Idibia

Legendary Award 2014- Yvonne Chaka Chaka

Transformational Leadership Award 2014- Chief Dr. Godswill Akpabio
Previous Post Next Post