Sarkodie, Tiwa Savage na Mafikizolo kuperform kwenye tuzo za BET

Majina ya wasanii watakaotumbuiza kwenye utoaji wa tuzo BET Experince mwaka huu zilizopewa yameanza kutangazwa.

Majina ya wasanii wakubwa wa Afrika yaliyotajwa ni pamoja na rapper kutoka Nigeria, Sarkodie, Tiwa Savage wa Nigeria na kundi la Mafikizolo la Afrika Kusini ambao watajumuika na wenzao kuperform Live katika jukwa hilo, Jumamosi, June 28 huko Los Angeles.



Hii ni mara ya kwanza kwa wasanii walio kwenye kipengele cha International acts kuperform katika tuzo hizo kubwa na zenye heshima zinazoandaliwa na kituo cha Black Entertainment Television (BET).

Diamond Platinumz kutoka Tanzania ni miongoni mwa wasanii wanaowania tuzo hizo kwa mwaka huu, na yuko katika kipengele cha Best International Act akiwa na Mafikizolo, Tiwa Savage, Davido, Sarkodie na Toofan.



Mchekeshaji Chris Rock na Emmy watakuwa hosts kwenye tuzo za BET mwaka huu ambazo zitaangaliwa zaidi na waafrika kulinganisha na miaka ya nyuma kutokana na ushirikishwaji wa ziada wa wasanii wa Afrika.
Previous Post Next Post