Ulevi wamponza mchumba wa Mase, soma hapa alichoambiwa na mume wake!

TMZ imeripoti kuwa rapper na pasta Mason Betha aka Mase amempiga marufuku mke wake kuingia na kuhubiri katika kanisa lake kutokana na kuwa mlevi.


Mase na Twlya

Uamuzi huo umefuatia baada ya mke wa Mase aitwaye Tylwa Betha zamani Twlya McInnis, kukamatwa na polisi akiwa anaendesha gari huku amelewa, na baada ya kupimwa damu yake ilikutwa na kilevi cha 14, mara mbili ya kiwango kinachoruhusiwa kwa mtu anayeendesha gari.

Inadaiwa kuwa Twyla amemtia sana aibu mume wake Mase kwa vitendo vyake kiasi cha kuwafanya hata wazee wa kanisa na waumini wengine waone mwanamke huyo ni mnafiki kusimama mbele yao na kuwahubiria kuwa ulevi ni dhambi.

Mase amesema kuwa Twlya amekuwa akitoa ushauri nasaha kwa watu wengine juu ya ndoa zao zinapokuwa na matatizo huku yak wake imemshinda, wawili hao maekuwa wakiishi tofauti toka mwaka 2012.

Previous Post Next Post