Lulu ashambuliwa baada ya kupost picha yake na ile ya Rihanna akiwa nusu 'mtupu'

Muigizaji wa bongo movies Elizabeth ‘Lulu’ Michael ambaye huonesha wazi jinsi anavyompenda Rihanna na hata kupoz kwenye jarida la VibeTz kama Rihanna kwenye jarida la GQ, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kupost picha ‘tata’ ya mwimbaji huyo kwenye Instagram.



Jana (April 29) Lulu alipost picha ya Rihanna aliyekava jarida la Lui akiwa amepozi na ameacha maziwa yake wazi huku akiwa na nguo ya ndani pekee.

“Abeeeee😳😳😳😳😳😳😳😳😳😳@badgalriri #Luicover.” Aliandika Lulu katika post ya picha hiyo.

Mtazazmo wa watu wengi haukuwa positive na walimshambulia kwa maneno makali huku na yeye akiitetea post yake na mara nyingine kutumia maneno makali (F-Words).

Hata hivyo, Lulu aliifuta post hiyo muda mfupi baadae kuepusha mengi..
Previous Post Next Post