Kiunyonge: Jay Z kuwa mpambe wa Kanye West kwenye harusi yake na Kim leo

Jay Z leo atakuwa mpambe wa Kanye West kwenye harusi yake na Kim Kardashian japo si kwa roho moja. Imedaiwa kuwa Jay anahisi harusi ya Kim Kardashian na Kanye West imepaniwa mno.


Kanye na Kim leo watafunga ndoa huko Florence nchini Italia. Kwa mujibu wa mtandao wa Radar Online, Jay anawapenda wawili hao lakini amekuwa akiwasema vibaya nyuma ya migongo yao.
Previous Post Next Post