Kim na Kanye wafunga ndoa, Jay Z na Beyonce washindwa kuhuzuria harusi yao!

Kim Kardashian amekuwa Mrs. West rasmi leo baada ya kufunga ndoa na Kanye West.

Mastaa hao wamefunga pingu za maisha kwenye harusi private iliyofanyika juu ya mlima Fort di Beleverdre huko Florence, Italia mbele za ndugu na marafiki zao.

KimKanye

Hata hivyo marafiki wakubwa wa Kanye, Jay Z na mke wake Beyonce hawakuwepo kwenye harusi hiyo.
Awali ilisemekana kuwa Jay Z angekuwa mpambe wa Kanye kwenye harusi hiyo kwakuwa wawili hao ni marafiki wa karibu.



Beyonce alipost picha hii muda ambao Kanye na Kim walikuwa wakifunga ndoa
Previous Post Next Post