Audio: Joh Makini aelezea jinsi Weusi wanavyopangilia projects zao

Weusi ni kundi bora la muziki Tanzania kwa mujibu wa KTMA 2014, lakini unaweza kukubaliana na Nikki wa Pili kuwa Weusi ndilo kundi bora zaidi la Hip Hop Afrika Mashariki kutokana na ubora wa kazi zao kila zinapotoka.



The Jump Off ya 100.5 Times Fm ilipiga story na Joh Makini ambaye alieleza jinsi ambavyo kundi hilo linafanya kazi zake na jinsi ambavyo wanaweza kuzipangilia projects za solo artists na za kundi.

“Sisi hatuoni kitu cha kutuzuia yaani, tunasukuma vitu vyote at the same time, tunasukuma Crew na solo projects at the same time.” Alisema Joh Makini.

Alisema project yake na Nick wa Pili (Joh Makini Vs Nick wa Pili) inaendelea kurekodiwa na kwamba project hiyo inarekodiwa tofauti na projects za kundi au solo projects.

Msikilize hapa akieleza kwa undani kuhusu jinsi wanavyomshirikisha Bonta katika projects ingawa yuko mbali na ushirikiano wao na producers mbalimbali.

Previous Post Next Post