Video: Jay Z na Nas waungana jukwaani na kuperform kwenye tamasha la Coachella,

Mahasimu wa zamani ambao ni magwiji wa hip hop, Jay Z na Nas waliwasurprise mashabiki waliohudhuria tamasha la Coachella linalofanyika Calfornia kwa wiki mbili mfululizo.



Wakati Nas akiendelea kuperform nyimbo zilizo kwenye albam yake ya Illmatic ambayo imetimiza miaka 20 hivi sasa, Jay Z alipanda pia jukwaani na kuimba verse ya ‘Dead President II na kisha kuhamia kwenye ‘Where I’m From’ kutoka kwenye albam yake In My Lifetime Vol.1.

Kabla hajaondoka jukwaaani alimpa shavu Nas.




“Peace to the god Nas! I had come all the way out here to celebrate 20 of Illmatic. What ana amazing accomplishment!”

Muda mfupi aliingia P. Diddy Puff Daddy ambaye kwa pamoja waliwasha moto na ‘Hate Me Now’.

Previous Post Next Post