Mabadiliko kwenye Twitter: Unaweza kupost picha 4 kwenye tweet moja na kutag watu hadi 10

Watumiaji wa mtandao wa kijamii wa Twitter wamezidi kuboreshewa na kurahisishiwa jinsi ya kuwasiliana na angalau kushare picha kunaanza kuwa kama Facebook.



Jana (March 26) kampuni hiyo imeongeza ‘features’ za Twitter ambapo mtumiaji anaweza kupost hadi picha 4 katika tweet moja, lakini kwa sasa hiyo inawezekana kwa watumiaji wanaotumia simu aina ya iPhone na baadae itawezekana kwenye aina nyingine za simu za kisasa (androids) na kwenye Twitter.com.

Lakini pia kwa mara ya kwanza watumiaji wa mtandao huo wanaweza kuwatag watu hadi 10 kwenye tweet moja yenye picha.
Previous Post Next Post