Angelina na Brad Pitt Jolie kuhamia Afrika Kusini kwa Ajili ya Kushoot Filamu Mpya

Mastaa wa filamu nchini Marekani Brad Pitt na Angelina Jolie watahamia nchini Afrika Kusini mwaka huu ambako watakuwa wakishoot filamu mpya.

































Angelina na Brad Pitt Jolie wenye watoto sita, wamepanga nyumba kwenye kitongoji cha Sandhurst jijini Johannesburg ambapo watakuwa wakilipa $7, 600 kwa mwezi. Gazeti la Beeld limesema wapenzi hao watakaa Afrika Kusini wakati Pitt atakuwa akiigiza filamu na George Clooney.

Haijulikani ni lini wataenda kuishi rasmi na kama watato wao wataungana nao pia.

Sio mara kwanza kwao kuishi Afrika. Mwaka 2006 walihamia Namibia ambako Jolie alijifungua mtoto wake wa kwanza, Shiloh Jolie-Pitt.
Previous Post Next Post