50 Cent kutoa album mpya June 2014,pia aachan na label ya Interscope

Rapper wa G-Unit Curtis Jackson maarufu kama 50 Cent ameachana rasmi na label ya Interscope aliyodumu nayo kwa maiak kumi na mbili , na kusaini dili mpya ya usambazaji na Caroline/Capitol/UMG katika maandalizi ya kutoa album yake mpya ‘Animal Ambition’ inayotarajiwa kutoka June 3.




“50 Cent is, and always will be, a marquee artist for us,” alisema Steve Berman, Vice Chairman wa Interscope/Geffen/A&M katika taarifa ya kuondoka kwa rapper huyo mzaliwa wa Queens.

Uongozi wa Interscope ulimtakia kila laheri katika ukurasa mpya alioufungua 50 Cent.
“We respect his decision to pursue this new venture and the next chapter in his career, and wish him nothing but the best. He will always be a part of our family.”

Fiddy aliwashukuru Dr. Dre pamoja na Eminem kwa kufanya nao kazi kwa kipindi chote hicho
“Nimepata mafanikio makubwa kwa kuwa na Shady/Aftermath/Interscope na pia ningependa kumshukuru Eminem na Dr. Dre kwa kunipa fursa hiyo, nimejifunza mengi kutoka kwao kwa miaka yote hiyo.”

Album mpya ya 50 inafuata baada ya ile ya mwaka 2009 ‘Before I Self Destruct’.

Previous Post Next Post