Wiz Khalifa Ampoteza Uncle Wake Baada Ya Kupigwa Risasi

Huko nchini Marekani Pittsburgh Waterfront imeripotiwa kuwa Uncle wa msanii wa miondoko ya Hip Hop, Rapper Wiz khalifa ameuwawa baada ya kupigwa risasi ya kichwa na watu wawili wenye weusi katika parking ya magari ya Steak ‘n Shake Waterfront. Imani Porter mwenye umri wa miaka 20 (Uncle wa Wiz Khalifah) alikuwa kwenye gari wakati wa tukio hilo na inasemekana kuwa Imani alikuwa nao katika gari watuhumiwa hao wawili kabla ya kumpiga risasi Imani.


Police wameripoti kuwa kwa sasa wanawatafuta watuhumiwa hao wawili ambao walionekana wakiondoka kwa mguu mara baada ya tukio hilo kuotokea na kisha walipofika mbele kidogo walipanda gari aina ya Pontiac Bonneville lenye rangi nyeupe. Msanii Wiz Khalifa kupitia mtandao wa twitter aliandika kuwa ameshangazwa na kusikitishwa na tukio hilo, Huku baba mzazi wa Imani akisema kuwa haishwi kututokwa na machozi kwa sasababu mwanae alikuwa bado mdogo.
Previous Post Next Post