Unajua ni Kwa Nini Rich Mavoko Aliimba Moyo Wangu? 'Msikilize Hapa'

Unaweza kuwa umeusikia wimbo wa Rich Mavoko mara nyingi lakini ukawa umeshindwa kuelewa maana yake ni nini licha ya kwamba ametumia Kiswahili. Hivi karibuni tulikaa na Rich Mavoko ambapo alituelezea maana halisi ya wimbo wake.


“Unaweza ukawa na msichana katika mapenzi naye lakini yule msichana unampenda kiasi ambacho kila kitu anachokifanya kwako wewe ni sawa. Lakini inafika kipindi anakufanyia mambo mengi maovu, unatamani uachane naye lakini huwezi kumwambia kwamba ‘achana na mimi’ au kumfukuza. Inapopatikana chance anaposema ‘mimi na wewe basi’ unasema ‘nashukuru Mungu bwana, bora aende zake aniachie roho yangu nisije nikafa,”alisema.



Previous Post Next Post