THE GAME AMUENZI NELSON MANDELA KWA KUJICHORA TATTOO


Hakuna mtu yoyote ambaye hajaguswa na kifo cha Mzee Nelson Mandela kutokana na historia ya pekee aliyoiacha kiongozi huyu wa Afrika Kusini.

Kuanzia mataifa ya Asia,Ulaya,Marekani, wanamichezo,waigizaji hadi watu wa kawaida wameonyesha masikitiko yao kwa kumpoteza mfano mzuri kwenye uongozi.

Headline mpya inamhusisha msanii nguli wa hiphop The Game ambaye ni mpenzi mkubwa wa tatoo. Hivi sasa amechora tatoo kubwa za sura za wanae,Barack Obama, Trayvon Martin na Nelson Mandela akiangalia nje ya gereza.


The game ali-share picha akionyesha tatoo hiyo kubwa na kuandika ,“The finished ‘Nelson Mandela’ lookin out of the prison bars by @NikkoHurtado done on my side. 7 hour sitting…. Few more hours to tie in the tats around it & we solid,”.


Kazi kwenu Tz artist na Afrika kwa Ujumla , Je utawezaje kumkumbuka Nelson  Mandela...?


Previous Post Next Post