Wanasayansi: Wanaume wenye sauti nzito huvutia zaidi wanawake, lakini sio

Najua Umeshawahi kujiuliza kwanini kipindi cha jioni cha East Africa Radio, East Africa Drive kinachoendeshwa na Flava, Big Easy cha Choice FM kinachoendeshwa na ML Chris ama Maskani cha Times FM kinachoendeshwa na Gadner G Habash vina wasikilizaji wengi wanawake? 

ML Chris, Choice FM

Ni kwasababu wanaume wenye sauti nzito huwavutia zaidi wanawake, utafiti umebaini.

Wanasayansi wamegundua kuwa wanaume wenye sauti nzito aka za kushiba, wanawavutia wanawake.. walau wale wanaotaka mahusiano ya muda mfupi.

Lakini bad news ni kuwa, wanaume wa aina hii ni rahisi mno kucheat na wameokana kuwa si waoaji. Utafiti uliochapishwa kwenye jarida la mtandaoni la Personality and Individual Differences, limetoa undani wa maendeleo ya sauti ya binadamu na uchaguzi wa mwenza.

‘Sauti ya mtu inaweza kuathiri jinsi tunavyowafikiria,’ Dr Jillian O’Connor, kutoka chuo kikuu cha McMaster cha Canada.
Previous Post Next Post