Update: Mtoto wa Usher Raymond aliyetaka kuzama kwenye bwawa la kuogelea aruhusiwa kutoka hospitali




Mtoto wa mwimbaji wa R&B Usher Raymond aitwaye Usher Raymond V aliyepata ajali ya maji wiki iliyopita amepona na kuruhusiwa kutoka hospitali.

Usher Raymond na Mtoto wake


uuu
Jana kamera za TMZ zilimuotea Usher Raymond V mwenye miaka 5 akiwa na bibi yake wakitoka katika moja ya sehemu za michezo ya watoto iitwayo Mighty Jumps iliyoko Atlanta, Marekani huku akiwa amefungwa bandage katika mkono wake wa kulia.
usher-2
Wiki moja iliyopita Usher Raymond V alinusurika kuzama katika bwawa la kuogelea lililoko nyumbani kwa baba yake lakini aliokolewa na kulazwa hospitali kwa siku kadhaa.

Previous Post Next Post