Ne-Yo atangaza kuachana na mchumba wake aliyezaa naye watoto wawili



Mara nyingi linapotokea jambo kwa msanii mkubwa katika kipindi ambacho anatarajia kutoa album au kufanya show huwa linaleta hisia za stunt ya kuvuta attention ya watu, kitu ambacho kimejitokeza kwa mwimbaji wa R&B Ne-Yo aliyetangaza kuachana na mchumba wake Monyetta mama wa watoto wake wawili kipindi ambacho anajiandaa kutoa album yake mpya.


Jumamosi iliyopita (June 29) Ne-Yo alipost picha (hapo juu) yenye ujumbe kuwa yeye na mchumba wake Monyetta Shaw wameachana kwa amani na kusema kuwa ataendelea kumpenda siku zote.

“The fate has decided to split our romantic paths, know that I will ALWAYS LOVE YOU. Forever your partner…Forever your friend.Forever my MIRACLE”. Huo ndio ujumbe ulioko katika picha aliyopost mkali huyo wa R&B ukimwendea mchumba wake.

Wakati Ne-yo anapost picha hiyo mchumba wake aliyekuwa Los Angeles, Marekani muda huo huo naye alipost picha akiwa na marafiki zake na wenye furaha (akiwa bado na pete ya uchumba ya Ne-Yo kidoleni) na akasindikiza picha hizo na tweet inayoonekana ni jibu ya ujumbe wa Ne-Yo “No worries! Got a gang of bad chick!!!! #girlpower #betweekend #letsgo #goodtimes”.



Previous Post Next Post