Sheria mpya ya kuzuia uvaaji wa suruali chini ya makalio maarufu kama ‘Kata K’ au ‘mlegezo’ imewakera ma rapper mbalimbali wa Marekani ambao wengi wao wameitafsiri kama kitendo cha kibaguzi ambacho serikali ya jiji la Wildwood imeamua kufanya.
![](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2013/06/game-sag.jpg)
Mmoja wa ma rapper waliokerwa na sheria hiyo mpya iliyopitishwa na jiji la Wildwood huko New Jersey Marekani ni The Game. Akiongea na mtandao wa TMZ Game ameonekana kuchukizwa na sheria hiyo na kusema kuwa hawawezi kuwapangia watu jinsi ya kuvaa nguo na kuongeza kuwa hizi sio enzi za utumwa. “They trying to get people to not sag, please. Can’t tell people how to wear their f***ing clothes. What time are we in? This ain’t the f***ing slave days. F*** that.”
Game aliongeza kuwa yeye ataendelea kuvaa mlegezo na watu watano wa kwanza kukamatwa kwa kosa hilo atawalipia faini yeye na ataenda huko huku akiwa amevaa kata K, “I am with the sagging movement. First five people to get fines, I will pay their tickets … I will go there and sag cause I am a sagging Sagittarius.”
![](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2013/06/mac-miller-bizzy-bone-getty.jpg)
Rapper mwingine aliyeonekana kutokubaliana na sheria hiyo ni Mac Miller ambaye hajatofautiana na Game na Bone kwa kusema huo ni ujinga na kuongeza kuwa yeye ataendelea kuvaa mlegezo popote aendapo, “I just think that’s ridiculous because no one has time to do that much community service. I sag and will sag anywhere I go.”
Sheria hiyo inategemewa kuanza kufanya kazi mwezi ujao (June) katika jiji la Wildwood, New Jersey nchini Marekani.