DIAMOND ASEMA WALIPAMGA KUFANYA HIT SONG NA NGWEA KAMA ANGELUDI SOUTH AFRICA





Hakika utakubaliana na mimi kwamba marehemu Albert Mangweha alikuwa ni miongoni mwa wasanii wakubwa sana kwa maana ya kukubalika kwa mashabiki na hata wasanii wenzake wa hip hop na hata wa kuimba.



Ikiwa ni siku moja kabla ya mwili wa marehemu Mangweha kuwasili Tanzania (June 2) tayari kwa mazishi, Diamond Platnumz naye amefunguka juu ya mpango waliokuwa nao yeye na Ngwea wa kufanya wimbo mpya hivi karibuni.

Kupitia akaunti yake ya Instagram Platnumz amesema yeye na Ngwair walikuwa na mpango wa kufanya wimbo mpya wa pamoja kama Ngwair angefanikiwa kurudi nyumbani Tanzania akiwa hai baada ya ziara yake ya Africa Kusini, kitu ambacho kwa bahati mbaya mwenyezi Mungu hakukipa baraka kwa sababu tunazoamini kuwa ni za heri pia.

Diamond ameandika maneno yafuatayo kupitia Akaunti yake ya  Instagram:

“Kinachoniuma zaidi ni jinsi tulivyokua tukijaribu kutengeneza HIT bila Mafanikio… si kwa
nyimbo niliyokushirikisha wala uliyonishirikisha, zote Hazikufikia Malengo yetu na Kuplan kufanya Ngoma Mpya Ukirudi toka South Africa…. bt pia kwa Mipango ya Mwenyez Mungu Haijawezekana… RIP Brother, I will always miss and Respect you.”
Previous Post Next Post

Popular Items