MAMBO SITA USIYOYAFAHAMU KUHUSU MUIGIZAJI WA BONGO MOVIE SNURA MUSHI




Mambo sita usiyoyafahamu kuhusu mwanadada Snura Mushi


Kufutia interview na mwandada Snura Mushi yafuatayo ni mambo sita ambayo huyafahamu kuhusu mwigizaji huyu mahiri wa bongo movies.


1. Snura alianza kuimba muziki kabla ya kujiingiza kwenye kuigiza na ashawahi kuwa mwimbaji wa taarabu.

2. Hupendelea kuvaa nguo ndefu na zinazoushika vizuri mwili wake kwani anaamani ana umbo zuri sana na anapendeza akivaa nguo ndefu na sio fupi.


3. Snura sio mpenzi wa kuzurura na hupendelea kukaa ndani muda mwingi akitazama Filamu mbalimbali za ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali


4. Hapendi kuzungumzia maisha ya mtu na ni mwanadada mpole na mstaarabu sana

5. Alishawahi kuandaa, kuigiza na kudirect movie aliyoiita “big sister” pamoja na mastaa wengine watano,ambayo baada ya kumaliza kuirekodi na kui “edit” ilipotea mikononi mwa producer na mpaka leo haijawahi kupatikana

6. Hapendelei sana kunywa pombe na huwa anakunywa kidogo sana
Previous Post Next Post