Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani akizunguma na viongozi Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) (kushoto) katika mkutano uliolenga kupata maoni ya kanisa hilo kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
Sheikh Ibrahim Ghulaam wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini akitoa maoni ya Baraza hilo kuhusu Katiba Mpya mbele ya Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa wa Karimjee Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa tarehe 11, Januari, 2013).
Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA), Kanda ya Mashariki Mchungaji Mark Malekana (kushoto) akitoa maoni ya kanisa lake kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013)