Mambo matano yatakayokugusa katika maisha ya diamond platnumz

Kila msanii anahistoria yake na maisha yake ya nyuma kaba ya kuwa msanii au kufikia mafanikio makubwa aliyoyapata haya ni mambo matano yanayomuhusu Diamond Platnumz aliyowai kuyapitia katika maisha yake yasome hapa

 


01. Diamond Platnumz aliachwa na baba yake


Diamond alizaliwa tarehe 2, October mwaka 1989 katika Hospitali ya Amana Dar es salaam. Akiwa na umri mdogo wazazi wake walitengana na baba yake kumuacha bila msaada wowote. Hapa chini huyo ndiyo baba yake diamond.



02. Chumba kupangishwa ili kumsomesha

Baada ya wazazi wake kutengana, Diamond aliamia kwa bibi yake huko tandale na ilipofika muda wa yeye kwenda sekondari ilibidi bibi yake apangishe chumba kimoja ili Diamond aende shule na ikabidi alale chumba kimoja na bibi na mama yake.



03. Aliacha shule kwa kukosa Ada

Diamond alikua na akili darasani na alipomaliza elimu yake ya O’level ilikosekana pesa ya kumpeleka A’level na hapo ndio ilikua mwisho wa elimu yake.




04. Diamond ameshafanya kazi viwandani, Kafanya kazi za kupigisha simu , kuuza mitumba na kuuza maji.

Kuna kipindi Diamond alikuwa akifanya kazi katika kiwanda cha mabegi kilichoko Mikocheni na kulipwa mashahara wa shilingi 2,000 kwa masaa 8.



05. Mama yake alisaidia sana kutoka kwake

Mama yake alikuwa anampeleka kwenye talent show na kumsubiria hadi usiku mpaka aperform ndo wanarudi wote. Ndugu zake wengine waliona anamdekeza mwanae.

Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA