Picha: Moe Musa kuongoza video mpya ya Diamond aliyomshirikisha Iyanya

Hii ndio Selfie aliyoipost Diamond kwenye ukurasa wake wa Instagram huenda ikategeua kitendawili cha ni wimbo upi staa huyo ameenda kushoot video yake nchini Uingereza.

Upande wa kushoto ni Iyanya na  Diamond, Babu Tale, Ommy Dimpoz, Moe Musa (wa pili kutoka kulia) na watu wengine wakiwa kwenye picha ya pamoja

Kama ilivyokuwa kwa Ommy Dimpoz(waliyesafiri naye hadi Uingereza) aliyemtumia muongozi wa video wa Uingereza, Moe Musa kushoot video ya wimbo wae Ndagushima, inaonekana Diamond naye ameamua kumtumia muongozaji huyo wa video za wasanii wengi maarufu wa Afrika.

Pia inavyoonekana wimbo unaofanyiwa video ni ule wa Diamond aliomshirikisha staa wa Kukere, Iyanya ambaye naye yupo kwenye selfie hiyo.

Moe Musa ameongoza video kibao zikiwemo Carol ya Star Boy f/ Wizkid, Azonto na Antenna za Fuse ODG, Skelewu ya Davido na zingine. Mambo yamekwiva!

Previous Post Next Post

Popular Items