Magari 30 ya Paul Walker yawekwa mnadani, jina lake kutotumika katika uuzaji

Watu wa karibu na familia ya aliyekuwa star wa Fast and Furious, marehemu Paul Walker wameamua kuuza magari 30 yaliyokuwa yanamilikiwa na star huyo.

Kwa mujibu wa TMZ, magari hayo ni pamoja na BMW, Audis, Musgangs na Porsches yakiwemo magari yanayotumika kwenye mashindano ya mbio za magari.



Hata hivyo, wameeleza kuwa hawatahusisha jina la Paul Walker na bidhaa zinazouzwa kwa kuwa wanaamini yeye pia asingependa kuona jina lake linatumika kufanya bei ya magari hayo iwe juu au kuvutia wateja zaidi.

Magari hayo yatauzwa kupitia mawakala maarufu wa minada.

Mali za Paul Walker zinakadiriwa kuwa na thamani ya $25 million na mtoto wake wa kike Meadow mwenye umri wa miaka 15 ndiye aliyetajwa na marehemu kuwa mrithi wa vitu vyote hivyo.

Wakati wa uhai wake, Paul alimtaka baba yake mzazi kusaidia katika kuhakikisha mwanae anahamishiwa mali hiyo.
Previous Post Next Post