Haya ndiyo Malipo utakayolipa kama ukimuitaji Moja kati ya wasanii hawa kutoka Nigeria

Unajua kwamba Diamond Platnumz aliwaza mbali mpaka kuamua kuanza kuutangaza muziki wake nchini Nigeria, na kuanza kufanya collabo na wasanii mastaa wa nchi hiyo sababu msanii akikubalika huko ni rahisi kuneemeka kwa shows za hela nyingi kama wanavyofaidi mastaa wa nchi hiyo.


Kwa sasa autoweza jiuliza tena ni  kwanini wasanii wengi wa Nigeria wanaishi maisha ya kifahari, jibu ni kuwa mbali na endorsement, pia wanatengeneza pesa ndefu sana kupitia show zao.

Mtandao wa Vanguard wa Nigeria umeandika kiasi cha pesa wanachotoza wasanii wa A-list wa Nigeria kwa show moja.

P-Square – M 150 Tshs
Mapacha wa P-Square Peter na Paul ndio wasanii wanaoonekana kutoza pesa nyingi zaidi, ili watumbuize katika show wanatoza kuanzia Naira milioni 8 hadi 15, sawa na Tshs milioni 81 hadi milioni 152 kwa show moja.

D’banj – Milioni 100 Tsh
Koko Master D’Banj anatoza kuanzia Naira M6 hadi 10 sawa na Tsh milioni 60 hadi M100 kwa show.

2 Face – Milioni 60 Tsh
2 Face Idibia anatoza kuanzia Naira milioni 5- 6 ambayo ni sawa na Tsh milioni 50 hadi milioni 60 kwa show moja.

Wizkid – M 50 Tshs
Wizkid hutoza kuanzia Naira milioni 4-5 sawa na Tshs milioni 40 hadi 50 kwa show.

Flavour – M 30 Tshs
Flavour huchukua Naira milioni 3 sawa na Tshs milioni 30 kwa show

Iyanya – M 30 Tshs
Kukere master Iyanya hutoza sawa na Flavour Naira milioni 3 sawa na Tshs milioni 30

Davido – M 35 Tshs
Davido ambaye pia ameshirikishwa katika Number 1 na Diamond Platnumz, hutoza Naira milioni 3 hadi 3.5 sawa na Tshs milioni 30 hadi 35 kwa show.

Tiwa Savage – M 25 Tshs
Tiwa Savage ambaye zamani akiwa Marekani alianza kwa kuwa backup singer kwa wasanii wakubwa kama Mary J na wengine, yeye huchaji Naira milioni 2.5 sawa na tshs milioni 25 kwa show.

Soma zaidi hapa kuna Orodha zaidi www.vanguardngr.com


Previous Post Next Post

Popular Items