Doh! Raper huyu akamatwa na Bhangi akiwa uwanja wa ndege, apiga picha akiwa yuko selo

Bila shaka utakuwa na shaka ya kutaka kujua ni rapper gani huyo aliyekamatwa na Bhangi? basi nakutoa shaka kwa kuanza kukupa full details


Rapper huyu ni Wiz Khalifa ambaye alikamatwa Jumapili hii asubuhi kwenye uwanja wa ndege huko Texas kwa kumiliki bangi.

Kwa mujibu wa TMZ, staa huyo alikuwa akisafiri kutoka El Paso kwenda Dallas pindi maafisa walipogundua amebeba majani. Alipelekwa na kuwekwa kwenye kituo cha polisi cha jirani ambako waligundua kuwa alikuwa na bangi. Hata hivyo rapper huyo wa “We Dem Boyz” alitweet selfie akiwa jela na kuandika:


“I wanna drop 28 Grams but they got me locced up. Soon as I get out, the tapes comin out. Fucc that.”
Aliligeuza tukio hilo kuwa trending topic kwa kuanzisha hashtag ya #FreeTrapWiz. “They’re tryna figure out how many grams I had. How ironic,” aliongeza.
Previous Post Next Post