Picha: Ommy Dimpoz ashoot video yake Mpya Nchini Uingereza na Director aliyefanya video ya ‘Caro’ ya Wizkid,na ‘Skelewu’ ya Davido

Makali anayehit na Miss Koi Koi Ommy Dimpoz anatarajia kuupeleka muziki wa Tanzania ‘next level’ baada ya wiki hii kushoot video ya wimbo wake mpya jijini London, Uingereza.

Video Queen atakayeonekana katika video mpya ya Ommy Dimpoz
Director Moe Musa akiwa kazini


































Ommy akiwa location ya video hiyo
Video hiyo imeongozwa na muongozaji wa video kutoka Nigeria anayeishi nchini Uingereza, Moe Musa. Muongozaji huyo ameongoza video za wasanii wengi wakubwa na nyimbo nyingi ni hits. Video hizo ni pamoja Azonto na Antenna za Fuse ODG, Skelewu ya Davido, Caro ya Starboy ft L.A.X na Davido, Ukwu ya Timaya na zingine nyingi.







































 Ommy Dimpoz ambaye amekuwa nchini Uingereza tangu Valentine’s Day, anatarajia kurudi nchini wiki ijayo na atajiandaa na ziara nyingine ya Muscat na Oman.






































Credit:Bongo5!
Previous Post Next Post

Popular Items