Barnaba kuanzisha Kipindi cha Television, Kuanza Juni mwaka Huu

Mwanamuziki Barnaba Elias 'Barnaba Boy Classic' anatarajaia kuanzisha kipindi kipya cha television  kitakachohusu maisha yake, kipindi hicho kinategemewa kuanza juni mwaka huu.

Barnaba kutoka Tanzania House of Talent (THT) amesema kuwa kipindi hicho kitaonyeshwa kupitia website yake na Youtube Page yake.



Akizungumza Barnaba alisema kipindi hicho kinachojulikana kama 'The Miracle Voice of Barnaba', kina lengo la kuwahabarisha mashabiki wake nini kinafanyika kila siku katika maisha ya Barnaba.

" Nipo katika harakati za kuanzisha kipindi changu kitakachozungumzia maisha ya Barnaba na kazi zake za kimuziki, amabacho nitakuwa nakirusha kwenye television kila wiki pia kitaweza kuonekana katika kurasa zangu za mitandao ya kijamii,kipindi hiki kitatoa fursa kwa sahabiki yoyote kukiangalia," Alisema Barnaba!
Previous Post Next Post