Ifahamu c9 Record kutoka kwa Producer C9

Jina lake halisi ni Charles Francis Charles mzaliwa wa Songea lakini amekaa sana Zanzibar. But ndani ya gemu la mziki wa Bongo fleva wengi tunamfahamu kama C9 wa Kili records. Kwa sasa C9 ana own music production studio yake iliyopo Togo street – Kinondoni Dar es salaam kiwa na jina la C9 Records.


Prodyuza huyo mwenye age ya 25 years ambaye ameshafanya hit nyingi na wasanii wakubwa akiwa na Kili records kama vile AT, the late Sharo milionea, Shilole, Rich mavoko etc, aliingia rasmi kwenye production mwaka 2009 mara baada ya kuhitimu masomo ya mziki huko Zanzibar eneo kwa mchina kwenye chuo cha Koinonia aliposoma kwa miaka 5.


“Imenichukua takribani miaka minne kuandaa studio yangu hii na hadi hapa ilipofika imenigharimu milioni 25 za kitanzania. Ni nguvu zangu mwenyewe ndo maana imenichukua muda mrefu kuiandaa na hakuna matarajio ya kufa leo wala kesho hapa.”- C9.

BK also wanted to know kwanini ameamua kufungua studio yake kwa gharama zote hizo badala ya kununua kiwanja au gari na changamoto anazokutana nazo baada ya kufungua studio yake.

“Kiukweli uprodyuza ni kitu kipo moyoni mwangu ndo maana nimeanza nayo na hivyo vingine vyote vitafuata ijapokuwa jambo hili limenigawa na baadhi ya watu waliotaka nisimiliki studio yangu ila sintowataja.”


Baabkubwa imepata fursa ya kutembelea studio hiyo na kujionea vyombo vya kisasa kabisa vilivyopo ndani ya studio hiyo ikiwa ni pamoja na kompyuta aina ya iMac, Kinanda kikubwa na cha kisasa kabisa, magita, mic zisizopugua tatu, eneo kubwa la studio lenye vyumba vikubwa kabisa vinne, full kiyoyozi, zuria safi n.k kwa ufupi kupo vizuri na tayari imeshafanya ngoma na wasanii wengi kama Amini, Nyamwela, Barnaba n.k.

Bongo61 Tunakutakia Mafanikio Mema C9.


Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA