SAMSUNG YAZIDI KUJIPANUA KATIKA TECHNOLOGY: YATENGENEZA TV YENYE UWEZO WA KUONYESHA CHANNELI MBILI KWA MPIGO ... BEI NI ZAIDI YA MILL 17

Kampuni yenye jina kubwa Duniani ya Sumsung Imezidi kujitanua zaidi hasa katika tecknolojia yake kwa kutengeneza Tv yenye  uwezo wa Kuonyesha Stesheni Mbili kwa Wakati Mmoja.Sasa aina maan kugombana tena kwani........


Samsung wameligundua hilo na ndio maana wametengeza TV (Samsung S9C OLED TV) inayoweza kuonesha channel mbili kwa wakati mmoja. Yaani maanake ni kuwa, ukiwa na TV hiyo unaweza kuendelea kufurahia kuangalia mechi ya Premier League na mkeo akiangalia tamthilia ya Mara Clara, hakuna tena mabishano.

Kwenye screen, vipindi viwili huonekana kwa kufifia lakini ukivaa miwani za 3D zilizotengenezwa na earphones zake, picha hujitenga na mmoja anaweza kuangalia mpira na mwingine kuangalia tamthilia ama kipindi kingine akipendacho.

TV hiyo inauzwa paundi 7,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 17.
Previous Post Next Post

Popular Items