PICHA: PICHA 3 ULIZOZIMISS KUTOKA INSTAGRAM

Msanii Na Mkali wa BongoFlavour Diamond Platinumz tayari ameshafika nchini Nigeria kwa ajili ya kazi ya kimuziki pamoja na wasanii nchini humo ambapo baada ya kufanya remix ya My Number One na Davido, kazi inaendelea na sasa amewafata hukohuko kwao Nigeria ili kufanya mambo mengi zaidi.




Diamond anaelezea kwamba baada ya kufanya ngoma na Davido, pia ngoma nyingine amefanya na Iyanya japokuwa watu wengi hawafahamu kuhusu hiyo collabo. Lengo lake kubwa lilikuwa si kufanya collabo tu bali anasema alitaka kujenga ukaribu na wasanii wa Nigeria ndiyo maana ameamua kwenda kufanya video hukohuko Nigeria.

Japokuwa hajasema ni production gani atatumia, hivi sasa Diamond ameshafika nchini Nigeria na atarudi baada ya kufanya video mbili ambapo moja akiwa na Davido na nyingine pamoja na Iyanya.

Msikilize hapa akizungumza na Millard Ayo.com




Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA