Mwanzo mzuri: Jack Wilshere alifunga bao la kwanza sekunde ya 29
Na Mahmoud Zubeiry.
MABAO mawili ya kiungo Jack Wilshere leo yameipa ushindi wa 2-0 Arsenal dhidi ya Marseille ya Ufaransa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Emirates.
Ilimchukua sekunde 29 tangu kuanza kwa mchezo huo kiungo huyowa England kufunga bao la kwanza akimtungua kipa hodari, Steve Mandanda na akfunga tena bao la pili dakika ya 65.
Kikosi cha Arsenal: Szczesny, Sagna, Monreal, Flamini, Mertesacker, Koscielny, Wilshere/Walcott dk75, Ramsey, Giroud, Ozil/Arteta dk82 na Rosicky/Cazorla dk75.
Marseille: Mandanda, Abdallah, Morel, Romao, N'Koulou, Lucas Mendes, J.Ayew/Valbuena dk57, Lemina/Cheyrou dk82, Gignac, Imbula/Thauvin dk57 na Khalifa.(P.T)




Katika mchezo mwingine, Chelsea imefungwa bao 1-0 na FC Basle, bao pekee la Mohamed Salah. Mabao ya Kaka dakika ya 12, Zapata dakika ya 49 na Balotelli dakika ya 59 yameipa AC Milan ushindi wa 3-0 dhidi ya Celtic nchini Scotland katika mchezo mwingine wa michuano hiyo.



Tags:
Sports