Askari wawili wa kulinda mbuga,pamoja na mwanajeshi mmoja wameuawa na waasi katika mbuga ya wanyama ya Virunga, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo .
Maafisa wanasema kuwa waasi watano pia waliuawa katika shambulizi ndani ya mbuga hiyo ambayo ndiyo iliyosalia pekee duniani kama hifadhi kwa sokwe.
Baadhi ya makundi ya waasi Mashariki mwa DRC ambayo yamejihami yana kambi zao katika msitu huo ambapo mara kwa mara huwinda wanyama kiharamu.
Kulingana na shirika la habari la Reuters waasi wa 23 ambao wana kambi zao humo, waliruhusu shughuli za kitalii kurejea katika hali ya kawaida.
Tags:
Social
